104 · Makkī

الهمزة

Al-Humaza·The Traducer

✦ memorize this sūrah

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

  1. وَيْلٌ لِّكُلِّ هُمَزَةٍ لُّمَزَةٍ﴿١﴾

    Ole wake kila safihi, msengenyaji!

  2. ٱلَّذِى جَمَعَ مَالًا وَعَدَّدَهُۥ﴿٢﴾

    Aliye kusanya mali na kuyahisabu.

  3. يَحْسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخْلَدَهُۥ﴿٣﴾

    Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

  4. كَلَّا لَيُنۢبَذَنَّ فِى ٱلْحُطَمَةِ﴿٤﴾

    Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.

  5. وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْحُطَمَةُ﴿٥﴾

    Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?

  6. نَارُ ٱللَّهِ ٱلْمُوقَدَةُ﴿٦﴾

    Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.

  7. ٱلَّتِى تَطَّلِعُ عَلَى ٱلْأَفْـِٔدَةِ﴿٧﴾

    Ambao unapanda nyoyoni.

  8. إِنَّهَا عَلَيْهِم مُّؤْصَدَةٌ﴿٨﴾

    Hakika huo utafungiwa nao

  9. فِى عَمَدٍ مُّمَدَّدَةٍۭ﴿٩﴾

    Kwenye nguzo zilio nyooshwa.

Quran Translation Name: Al-Barwani Translator: Ali Muhsin Al-Barwani Language: Swahili ID: sw.barwani Last Update: August 16, 2010 Source: Tanzil.net

Play surah