95 · Makkī

التين

At-Tin·The Fig

✦ memorize this sūrah

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

  1. وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيْتُونِ﴿١﴾

    Naapa kwa tini na zaituni!

  2. وَطُورِ سِينِينَ﴿٢﴾

    Na kwa Mlima wa Sinai!

  3. وَهَٰذَا ٱلْبَلَدِ ٱلْأَمِينِ﴿٣﴾

    Na kwa mji huu wenye amani!

  4. لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ فِىٓ أَحْسَنِ تَقْوِيمٍ﴿٤﴾

    Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.

  5. ثُمَّ رَدَدْنَٰهُ أَسْفَلَ سَٰفِلِينَ﴿٥﴾

    Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!

  6. إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ﴿٦﴾

    Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.

  7. فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعْدُ بِٱلدِّينِ﴿٧﴾

    Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?

  8. أَلَيْسَ ٱللَّهُ بِأَحْكَمِ ٱلْحَٰكِمِينَ﴿٨﴾

    Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?

Quran Translation Name: Al-Barwani Translator: Ali Muhsin Al-Barwani Language: Swahili ID: sw.barwani Last Update: August 16, 2010 Source: Tanzil.net

Play surah