101 · Makkī

القارعة

Al-Qaari'a·The Calamity

✦ memorize this sūrah

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

  1. ٱلْقَارِعَةُ﴿١﴾

    Inayo gonga!

  2. مَا ٱلْقَارِعَةُ﴿٢﴾

    Nini Inayo gonga?

  3. وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْقَارِعَةُ﴿٣﴾

    Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?

  4. يَوْمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلْفَرَاشِ ٱلْمَبْثُوثِ﴿٤﴾

    Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;

  5. وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ ٱلْمَنفُوشِ﴿٥﴾

    Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!

  6. فَأَمَّا مَن ثَقُلَتْ مَوَٰزِينُهُۥ﴿٦﴾

    Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,

  7. فَهُوَ فِى عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ﴿٧﴾

    Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.

  8. وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَٰزِينُهُۥ﴿٨﴾

    Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,

  9. فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٌ﴿٩﴾

    Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!

  10. وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا هِيَهْ﴿١٠﴾

    Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?

  11. نَارٌ حَامِيَةٌۢ﴿١١﴾

    Ni Moto mkali!

Quran Translation Name: Al-Barwani Translator: Ali Muhsin Al-Barwani Language: Swahili ID: sw.barwani Last Update: August 16, 2010 Source: Tanzil.net

Play surah