100 · Makkī

العاديات

Al-Aadiyaat·The Chargers

✦ memorize this sūrah

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

  1. وَٱلْعَٰدِيَٰتِ ضَبْحًا﴿١﴾

    Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,

  2. فَٱلْمُورِيَٰتِ قَدْحًا﴿٢﴾

    Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,

  3. فَٱلْمُغِيرَٰتِ صُبْحًا﴿٣﴾

    Wakishambulia wakati wa asubuhi,

  4. فَأَثَرْنَ بِهِۦ نَقْعًا﴿٤﴾

    Huku wakitimua vumbi,

  5. فَوَسَطْنَ بِهِۦ جَمْعًا﴿٥﴾

    Na wakijitoma kati ya kundi,

  6. إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٌ﴿٦﴾

    Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!

  7. وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌ﴿٧﴾

    Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!

  8. وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلْخَيْرِ لَشَدِيدٌ﴿٨﴾

    Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!

  9. أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِى ٱلْقُبُورِ﴿٩﴾

    Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?

  10. صفحة ٦٠٠
  11. وَحُصِّلَ مَا فِى ٱلصُّدُورِ﴿١٠﴾

    Na yakakusanywa yaliomo vifuani?

  12. إِنَّ رَبَّهُم بِهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّخَبِيرٌۢ﴿١١﴾

    Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!

Quran Translation Name: Al-Barwani Translator: Ali Muhsin Al-Barwani Language: Swahili ID: sw.barwani Last Update: August 16, 2010 Source: Tanzil.net

Play surah