86 · Makkī

الطارق

At-Taariq·The Morning Star

✦ memorize this sūrah

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

  1. وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ﴿١﴾

    Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!

  2. وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ﴿٢﴾

    Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?

  3. ٱلنَّجْمُ ٱلثَّاقِبُ﴿٣﴾

    Ni Nyota yenye mwanga mkali.

  4. إِن كُلُّ نَفْسٍ لَّمَّا عَلَيْهَا حَافِظٌ﴿٤﴾

    Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.

  5. فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ﴿٥﴾

    Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?

  6. خُلِقَ مِن مَّآءٍ دَافِقٍ﴿٦﴾

    Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,

  7. يَخْرُجُ مِنۢ بَيْنِ ٱلصُّلْبِ وَٱلتَّرَآئِبِ﴿٧﴾

    Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.

  8. إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجْعِهِۦ لَقَادِرٌ﴿٨﴾

    Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.

  9. يَوْمَ تُبْلَى ٱلسَّرَآئِرُ﴿٩﴾

    Siku zitakapo dhihirishwa siri.

  10. فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٍ وَلَا نَاصِرٍ﴿١٠﴾

    Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.

  11. وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجْعِ﴿١١﴾

    Naapa kwa mbingu yenye marejeo!

  12. وَٱلْأَرْضِ ذَاتِ ٱلصَّدْعِ﴿١٢﴾

    Na kwa ardhi inayo pasuka!

  13. إِنَّهُۥ لَقَوْلٌ فَصْلٌ﴿١٣﴾

    Hakika hii ni kauli ya kupambanua.

  14. وَمَا هُوَ بِٱلْهَزْلِ﴿١٤﴾

    Wala si mzaha.

  15. إِنَّهُمْ يَكِيدُونَ كَيْدًا﴿١٥﴾

    Hakika wao wanapanga mpango.

  16. وَأَكِيدُ كَيْدًا﴿١٦﴾

    Na Mimi napanga mpango.

  17. فَمَهِّلِ ٱلْكَٰفِرِينَ أَمْهِلْهُمْ رُوَيْدًۢا﴿١٧﴾

    Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.

Quran Translation Name: Al-Barwani Translator: Ali Muhsin Al-Barwani Language: Swahili ID: sw.barwani Last Update: August 16, 2010 Source: Tanzil.net

Play surah