90 · Makkī

البلد

Al-Balad·The City

✦ memorize this sūrah

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

  1. لَآ أُقْسِمُ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ﴿١﴾

    Naapa kwa Mji huu!

  2. وَأَنتَ حِلٌّۢ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ﴿٢﴾

    Nawe unaukaa Mji huu.

  3. وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ﴿٣﴾

    Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.

  4. لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ فِى كَبَدٍ﴿٤﴾

    Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

  5. أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ﴿٥﴾

    Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?

  6. يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُّبَدًا﴿٦﴾

    Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

  7. أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ﴿٧﴾

    Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

  8. أَلَمْ نَجْعَل لَّهُۥ عَيْنَيْنِ﴿٨﴾

    Kwani hatukumpa macho mawili?

  9. وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ﴿٩﴾

    Na ulimi, na midomo miwili?

  10. وَهَدَيْنَٰهُ ٱلنَّجْدَيْنِ﴿١٠﴾

    Na tukambainishia zote njia mbili?

  11. فَلَا ٱقْتَحَمَ ٱلْعَقَبَةَ﴿١١﴾

    Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

  12. وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْعَقَبَةُ﴿١٢﴾

    Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

  13. فَكُّ رَقَبَةٍ﴿١٣﴾

    Kumkomboa mtumwa;

  14. أَوْ إِطْعَٰمٌ فِى يَوْمٍ ذِى مَسْغَبَةٍ﴿١٤﴾

    Au kumlisha siku ya njaa

  15. يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ﴿١٥﴾

    Yatima aliye jamaa,

  16. أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ﴿١٦﴾

    Au masikini aliye vumbini.

  17. ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْمَرْحَمَةِ﴿١٧﴾

    Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

  18. أُو۟لَٰٓئِكَ أَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ﴿١٨﴾

    Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

  19. وَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا هُمْ أَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ﴿١٩﴾

    Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

  20. عَلَيْهِمْ نَارٌ مُّؤْصَدَةٌۢ﴿٢٠﴾

    Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.

Quran Translation Name: Al-Barwani Translator: Ali Muhsin Al-Barwani Language: Swahili ID: sw.barwani Last Update: August 16, 2010 Source: Tanzil.net

Play surah